Mashangilio 87

Mashangilio 87

Kuutukuza mji wa Sioni.

1Ulijengwa na kushikizwa kwenye milima iliyo mitakatifu.

2Bwana huipenda milango wa Sioni kuliko makao yote ya Yakobo.

3Mambo yenye utukufu hutangazwa mwako ulio mji wa Mungu.

4Nitakumbusha Rahabu na Badeli miongoni mwao wanijuao, waliozaliwa mumo humo watazameni: wamo Wafilisti na Watiro, hata Wanubi![#Yes. 30:7; Sh. 68:32; 89:11.]

5Sioni hutukuzwa kwamba: Watu wa makabila yote huzaliwa mle! Naye Alioko huko juu ndiye anayeushupaza.

6Bwana akiyahesabu makabila ya watu ataandika kwamba: Fulani na fulani walizaliwa mlemle.

7Nao wenyewe watacheza ngoma pamoja na kuimba: Visima vyangu vyote vimo mwako!

Swahili Roehl Bible 1937 © Bible Society of Tanzania, 1937.
Published by: Bible Society of Tanzania