The chat will start when you send the first message.
1Waovu hukimbia wasipofuatiwa na mtu;
Bali wenye haki ni wajasiri kama simba.
2Kwa sababu ya maasi ya nchi wakuu wake huwa wengi;
Bali kwa wenye ufahamu na maarifa hali ya nchi hudumishwa
3Mtu mhitaji awaoneaye maskini,[#Mt 18:28]
Ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza chakula.
4Wao waiachao sheria huwasifu waovu;[#1 Fal 18:18; Mt 3:7; Efe 5:11; 1 Tim 5:20]
Bali wao waishikao hushindana nao.
5Watu waovu hawaelewi na haki;[#Yn 7:17]
Bali wamtafutao BWANA huelewa na zote.
6Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake,
Kuliko mpotovu wa njia angawa ni tajiri.
7Yeye aishikaye sheria ni mwana mwenye hekima;
Bali aliye rafiki wa walafi humwaibisha babaye.
8Yeye azidishaye mali yake kwa riba na faida,
Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.
9Yeye aligeuzaye sikio lake asiisikie sheria,[#2 Tim 4:3; Zab 66:18; Lk 13:25-27]
Hata sala yake ni chukizo.
10Kila mtu awapotezaye wenye haki katika njia mbaya,[#Zab 34:9,10; Mt 6:33; Mk 10:30; Lk 18:29,30; Rum 8:32; 1 Kor 3:22,23]
Ataanguka katika rima lake mwenyewe;
Bali wakamilifu watarithi mema.
11Mtu tajiri ana hekima machoni pake mwenyewe;
Bali maskini mwenye ufahamu humchunguza sana.
12Wenye haki washindapo, uko utukufu mwingi;
Bali waovu waondokapo, watu hujificha.
13Afichaye dhambi zake hatafanikiwa;
Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.
14Mwanadamu mwenye kicho yu heri sikuzote;
Bali mshupavu wa moyo ataangukia madhara.
15Kama simba angurumaye, na dubu mwenye njaa;[#Mt 2:16]
Ndivyo alivyo mtu mbaya awatawalaye maskini.
16Mkuu aliyepungukiwa na akili huwaonea watu sana;
Bali achukiaye kutamani ataongeza siku zake.
17Aliyelemewa na damu ya mtu
Atalikimbilia shimo; wala mtu asimzuie.
18Aendaye kwa unyofu ataokolewa;
Bali mkaidi wa njia zake ataanguka mara.
19Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele;
Bali afuataye mambo ya upuzi atapata umaskini wa kumtosha.
20Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele;
Lakini afanyaye haraka kuwa tajiri hakosi ataadhibiwa.
21Kupendelea watu si kwema;[#Eze 13:19]
Wala mtu kuasi kwa ajili ya kipande cha mkate.
22Mwenye husuda afanya haraka kuwa tajiri;
Wala haufikiri uhitaji utakaomjia.
23Amkemeaye mwenzake hatimaye atapata kibali;
Zaidi ya mtu ajipendekezaye kwa ulimi wake.
24Aibaye mali ya babaye au mamaye, na kusema, Si kosa;
Mwana huyo ni rafiki wa mtu mharibifu.
25Mwenye nafsi ya kutamani huchochea fitina;[#1 Tim 6:6]
Bali amtumainiye BWANA ataneemeshwa.
26Mwenye kujitumainia moyo wake ni mjinga;
Bali yeye aendaye kwa busara ataokolewa.
27Mwenye kuwagawia maskini hatahitaji kitu;
Bali afichaye macho yake atakuwa na laana nyingi.
28Wasio haki wainukapo, wanadamu hujificha;
Bali waangamiapo, wenye haki huongezeka.