The chat will start when you send the first message.
1Unirehemu, Ee Mungu, unirehemu mimi,[#Isa 26:20]
Maana nafsi yangu imekukimbilia Wewe.
Nitaukimbilia uvuli wa mbawa zako,
Hadi misiba hii itakapopita.
2Nitamwita MUNGU Aliye Juu,[#Zab 138:8]
Mungu anitimiziaye mambo yangu.
3Atanitumia msaada toka mbinguni na kuniokoa,[#Zab 144:5; 40:11]
Atawaaibisha wale wanaotaka kunishambulia.
Mungu atazituma
Fadhili zake na kweli yake.
4Nafsi yangu i kati ya simba,[#Mit 30:14; Zab 64:3]
Nitastarehe kati yao waliowaka moto.
Wanadamu meno yao ni mikuki na mishale,
Na ndimi zao ni upanga mkali.
5Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,[#Zab 108:5]
Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako.
6Wameweka wavu ili kuninasa miguu;[#Zab 9:15]
Nimevunjika moyo;
Wamechimba shimo njiani mwangu;
Lakini wao wenyewe wametumbukia humo!
7Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti,[#Zab 108:1]
Moyo wangu ni thabiti.
Nitaimba, nitaimba kwa sauti nzuri,
8Amka, ee moyo wangu.[#Amu 5:12]
Amka, kinanda na kinubi,
Nitaamka alfajiri.
9Ee Bwana, nitakushukuru kati ya watu,
Nitakuimbia sifa kati ya mataifa.
10Maana fadhili zako ni kubwa hata mbinguni,[#Zab 108:4]
Na uaminifu wako hata mawinguni.
11Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,
Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako.