Zaburi 61

Zaburi 61

Hakikisho la ulinzi wa Mungu

1Ee Mungu, ukisikie kilio changu,

Uyasikilize maombi yangu.

2Toka mwisho wa nchi nitakulilia ninapozimia moyo,[#1 Tim 2:8]

Uniongoze juu ya mwamba nisioweza kuupanda.

3Kwa maana ulikuwa kimbilio langu,[#Mit 18:10]

Ngome yenye nguvu adui asinipate.

4Nitakaa katika hema yako milele,[#Zab 15:1; 23:6; Ufu 3:12]

Na kupata kimbilio chini ya mbawa zako.

5Maana Wewe, Mungu, umezisikia nadhiri zangu.[#1 Kor 3:21-23]

Umewapa urithi wao waliogopao jina lako.

6Utaziongeza siku za mfalme,

Miaka yake itakuwa kama vizazi vingi.

7Atakaa mbele za Mungu milele,[#Zab 41:12; Lk 1:32]

Ziagize fadhili na kweli zimhifadhi.

8Ndivyo nitakavyoliimbia jina lako daima,[#Zab 56:12]

Ili niondoe nadhiri zangu kila siku.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya