Ayu 25

Ayu 25

Bildadi Anena: Mtu Awezaje kuwa Mwenye Haki Mbele za Mungu

1Ndipo Bildadi, Mshuhi, akajibu, na kusema,

2Enzi na hofu zi pamoja naye;

Hufanya amani katika mahali pake palipoinuka.

3Je! Majeshi yake yahesabika?[#Mwa 1:3-5,14-16; Zab 19:4-6; 139:8,11; Mt 5:45; Yak 1:17]

Ni nani asiyetokewa na mwanga wake?

4Basi mtu awezaje kuwa na haki mbele ya Mungu?[#Ayu 4:17; 9:2; Zab 130:3; 143:2; Rum 3:19,20]

Au awezaje kuwa safi aliyezaliwa na mwanamke?

5Tazama, hata mwezi hauangazi,

Wala nyota si safi machoni pake;

6Siuze mtu, aliye mdudu![#Zab 22:6]

Na mwanadamu, ambaye ni buu!

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania