Zab 15

Zab 15

Nani Atakaa katika Patakatifu pa Mungu?

1BWANA, ni nani atakayekaa[#Zab 2:5]

Katika hema yako?

Ni nani atakayefanya maskani yake

Katika kilima chako kitakatifu?

2Ni mtu aendaye kwa ukamilifu,[#Zab 84:11; Isa 33:15,16]

Na kutenda haki.

Asemaye kweli kwa moyo wake,

3Asiyesingizia kwa ulimi wake.

Wala hakumtenda mwenziwe mabaya,

Wala hakumsengenya jirani yake.

4Machoni pake mtu asiyefaa hudharauliwa,[#Yos 9:18-20]

Bali huwaheshimu wamchao BWANA

Ingawa ameapa kwa hasara yake,

Hayabadili maneno yake.

5Hakutoa fedha yake apate kula riba,[#Eze 18:8,9]

Hakutwaa rushwa amwangamize asiye na hatia.

Mtu atendaye mambo hayo

Hataondoshwa milele.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania