Zab 99

Zab 99

Sifa kwa Utukufu wa Mungu

1BWANA ametamalaki, mataifa wanatetemeka;[#Kut 25:22]

Ameketi juu ya makerubi, nchi inatikisika.

2BWANA katika Sayuni ni mkuu,

Naye ametukuka juu ya mataifa yote.

3Na walishukuru jina lake kuu la kuhofiwa;[#Kum 28:58; Isa 6:3; Ufu 4:8]

Ndiye mtakatifu.

4Nguvu za mfalme nazo zapenda hukumu;[#Kum 32:3,4; Ayu 36:5; Isa 11:3-5; Yer 23:5; Mwa 18:25]

Wewe ndiwe uliyeithibitisha adili;

Ulifanya hukumu na haki katika Yakobo.

5Mtukuzeni BWANA, Mungu wetu;[#1 Nya 28:2; Zab 132:7; Isa 66:1]

Sujuduni penye kiti cha miguu yake;

Ndiye mtakatifu.

6Musa na Haruni miongoni mwa makuhani wake,

Na Samweli miongoni mwao waliitiao jina lake,

Walipomwita Bwana aliwaitikia;

7Katika nguzo ya wingu alikuwa akisema nao.[#Kut 19:9; Kut 33:9; Hes 12:5]

Walishika shuhuda zake na amri aliyowapa.

8Ee BWANA, Mungu wetu, ndiwe uliyewajibu;[#Hes 14:20; Sef 3:7; Kum 9:20]

Ulikuwa kwao Mungu mwenye kusamehe

Ingawa uliwapatiliza matendo yao.

9Mtukuzeni BWANA, Mungu wetu;

Sujuduni mkiukabili mlima wake mtakatifu;

Maana BWANA, Mungu wetu, ndiye mtakatifu.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania